|  
                     PROCEDURES 
                    FOR REGISTRATION OF NON GOVERNMENTAL ORGANIZATIONS UNDER THE 
                    NON GOVERNMENTAL ORGANIZATIONS ACT, NO. 24/2002 
                  TARATIBU ZA USAJILI WA NGOs 
                    CHINI YA SHERIA YA MASHIRIKA YASIYO YA KISERIKALI (NGOs) NA. 
                    24 YA MWAKA 2002 
                  Maombi ya usajili wa Mashirika Yasiyo 
                    ya Kiserikali yatakuwa na viambatanisho vifuatavyo kama ilivyopendekezwa 
                    na Sheria hii katika kifungu cha 12(2) 
                  a) Katiba ya Shirika lisilo la Kiserikali 
                    b) Taarifa yenye majina na saini za wanachama waanzilishi 
                    c) Maelezo binafsi ya wanachama na picha 
                    d) Ada ya usajili 
                    e) Anuani na sehemu yalipo makao makuu ya ofisi za Shirika 
                    Lisilo la Kiserikali 
                    f) Maelezo yoyote au taarifa kama itakavyohitajiwa na Msajili 
                  Maombi ya usajili wa Shirika Lisilo la 
                    Kiserikali yatakuwa kwenye fomu maalum NGO A form No. 1 
                    Maombi ya Cheti cha ukubalifu (certificate of Compliance) 
                    yatakuwa na viambatanisho vifuatavyo: - 
                  a) Kivuli halisi cha Katiba ya Shirika 
                    Lisilo la Kiserikali. 
                    b) Cheti cha usajili chini ya Sheria nyingine tofauti na Sheria 
                    ya Mashirika Yasiyo ya Kiserikali. 
                    c) Taarifa yenye majina na saini za wanachama waanzilishi. 
                    d) Maelezo binafsi ya wanachama na picha 
                    e) Anuani na sehemu yalipo makao makuu ya ofisi za Shirika 
                    Lisilo la Kiserikali. 
                    f) Maelezo yoyote au taarifa kama itakavyohitajiwa na Msajili. 
                     
                    Maombi ya Cheti cha ukubalifu yatakuwa kwenye fomu maalum 
                    NGO A form No, 3. 
                  ADA 
                    Ada ya usajili ngazi ya Wilaya itakuwa ni Shs 41,500/= kama 
                    ifuatavyo: 
                    - Ada ya faili 15,000/ = 
                    - Ada ya usajili 25,000/= 
                    - Stamp duty 1,500/= 
                  Ada ya usajili ngazi ya Mkoa itakuwa ni 
                    Shs 56,500/= kama ifuatavyo: 
                    - Ada ya faili 15,000/= 
                    - Ada ya usajili 40,000/= 
                    - Stamp duty 1,500/= 
                  Ada ya usajili ngazi ya Taifa itakuwa 
                    ni Shs 66,500/= kama ifuatavyo: 
                    - Ada ya faili 15,000/= 
                    - Ada ya usajili 50,000/= 
                    - Stamp duty 1,500/=  
                  Ada ya Mashirika ya Kimataifa itakuwa 
                    ni USD 267 kama ifuatavyo: 
                    - Adayafaili US$ 15 
                    - Ada ya usajili US$ 250 
                    - Stamp duty US$ 2 
                     
                    Kila Shirika lisilo la Kiserikali lililosajiliwa na kupatiwa 
                    cheti cha ukubalifu chini ya Sheria hii, linatakiwa kulipa 
                    ada ya mwaka ya Shs. 50,000/= au US$ 60 kwa Mashirika ya Kimataifa. 
                    Mashirika haya pia yatapaswa kuwasilisha taarifa zake za kazi 
                    za kila mwaka (Annual Report) ambazo zitakuwa kwenye Fomu 
                    maalumu NGO A Form Na. 10 kwa Msajili Mkuu kupitia kwa Wasajili 
                    Wasaidizi. 
                    Mashirika ya Kitaifa na Kimataifa yatasajiliwa moja kwa moja 
                    na Msajili Mkuu. Taratibu zake zitakuwa kama zilivyo taratibu 
                    za usajili katika ngazi nyingine isipokuwa kutakuwa na tofauti 
                    katika ada ya usajili, halikadhalika maombi ya usajili katika 
                    ngazi hizi yatawasilishwa moja kwa moja kwa Msajili Mkuu. 
                  MAMBO MBALIMBALI YA KUZINGATIWA 
                    Utaratibu wa malipo ya ada ya usajili/ mwaka 
                    Malipo ya ada ya usajili wa NGOs na ada za mwaka 
                    yatafanyika kama ifuatavyo: 
                     
                    (i) NGOs zote zitakazosajili katika ngazi ya Mikoa na Wilaya 
                    watalipa fedha katika Akaunti Nambari 16:29 Miscellaneous 
                    Deposit (Akaunti hii ni ya Hazina iliyoko kila mkoa) kwenye 
                    matawi ya Benki ya NMB katika maeneo yao. 
                     
                    (ii) NGOs zitakazosajili ngazi ya 
                    Kitaifa na Kimataifa watalipa fedha zao katika Akaunti Nambari 
                    16:140 Miscellaneous Deposit (Hazina Ndogo mkoa wa Dar es 
                    Salaam). Kiutendaji Idara ya Uhasibu, Ofisi ya Makamu wa Rais 
                    itapokea fedha hizo na kutoa stakabadhi halali ya malipo hayo. 
                       |